Skip to main content

Posts

kilimo cha nyanya

 Upungufu wa madini muhimu  Ili nyanya iweze kustawi vizuri katika kila hatua yake ya ukuaji inahitaji virutubisho au madini muhimu, Panapokosekana madini hayo au virutubisho hivyo nyanya huweza kuonyesha dalili mbalimbali za upungufu wa madini husika. Yafuatayo ni madini au virutubisho na dalili zake endapo zitakosekana katika zao la nyanya. 1) Madini ya nitrogen (N) Ni madini muhimu kwa ajili ya ukuaji hasa utengenezaji wa majani ya rangi ya kijani kibichi. Madini haya huitajika sana wiki chache baada ya kupandikiza. Rangi ya kijani ni muhimu kwa nyanya na hata kwa mazao mengine ili mmea uweze kutengeneza chakula chake. Naitrogeni inapokosekana katika mmea rangi ya kijani hupauka na kuwa njano na hatimaye mmea kudumaa. Pia naitrogeni inapotumika kwa wingi kupita kiasi husababisha mmea kuwa na majani mengi bila ya matunda na hivyo kuathiri matunda. Kunapokuwa na upungufu wa naitrogeni inashauriwa kutumia mbolea za chumvi kama CAN, UREA, SA na NPK. 2)Madini ya fosforasi (P) Ni madini m

Kilimo cha nyanya

 Magonjwa ya nyanya 1)Bakajani wahi ( Early blight) Ni ugonjwa wa fangasi ni ukungu unaoshambulia mimea ya nyanya kwa kiasi kikubwa. Ugonjwa huu hushambulia zaidi katika kipindi cha mvua. Dalili za ugonjwa huu ni kua na madoa madogo madogo yenye rangi nyeusi au rangi ya kahawia kwenye majani hasa ya chini, matunda na shina. Miche midogo kwenye kitalu inaposhambuliwa hunyauka na kufa, na Miche mikubwa hudondosha majani na matunda na kunyauka kwa shina na hatimaye kufa. Udhibiti Hakikisha Usafi wa shamba na ng'oa masalia ya mazao na kuchoma moto mara moja baada ya kuvuna. Pia zingatia mzunguko wa mazao na pia tumia mbegu ambazo hupinga ugonjwa huu(Resistant varieties) . Viuatilifu ambavyo vinaweza kutumika ni kama vile EVITO T 477 SC, GLORY 750 WG (MANCOZEB), CUPROCAFFARO 50 WP (COPPER OXYCHLORIDE) 2)Bakajani chelewa (Late blight) Ni ugonjwa  hatari sana haswa kipindi cha mvua na baridi ya wastani. Dalili za ugonjwa huu ni kuwa na mabaka makubwa yenye majimaji kwenye matunda, Shina n

Kilimo cha nyanya

 Utangulizi Zao la nyanya ni zao ambalo hulimwa dunia nzima.Kwa Tanzania zao la nyanya hutumika katika matumizi ya kila siku ya chakula.Nyanya ni miongoni mwa zao la mboga mboga inayopatikana katika jamii ya solanaceae,mazao mengine maarufu yanayopatikana katika jamii hii ni pilipili hoho,bilinganya,nyanya chungu na viazi mviringo.Pia zao la nyanya limeonekana kutengeneza pesa nyingi kuliko mazao mengine yalioko katika jamii hiyo ya solanaceae hivyo huweza kuinua uchumi wa mkulima.Pia zao la nyanya linahitaji umakini mkubwa katika matumizi ya pembe jeo.       Hali ya hewa Nyanya hustawi vizur katika hali ya hewa yenye nyuzi joto Kati ya 21-32C.Kiwango cha maji ambacho kinahitajika ni 1880mm kwa msimu mzima.Kwa maana hiyo nyanya huweza kustawi katika maeneo ya joto kuliko katika maeneo ya baridi.      Udongo Nyanya hukua vizuri katika udongo tifutifu wenye rutuba ambao hautuamishi maji,pia huweza kustawi katika udongo mfinyanzi na kichanga.kiasi cha pH ya udongo inayohitajika katika zao

Maliasili zetu

Utangulizi Kwa kawaida ni muhimu kukijua kitu kabla ya kukifanya au kukitumia. Ndugu msomaji karibu upate kujifunza kuhusu maliasili. Katika hii dunia, kila nchi ina maliasili zake japo tunatofautiana kwa uwingi na aina ya maliasili hizo. Na Tanzania kama nchi, tunazo maliasili nyingi sana ambazo zinatusaidia katika Maisha yetu ya kila siku. Maliasili ni nini? Maliasili ni rasilimali asilia zinazopatikana kwenye nchi husika, kwa upande wetu, ni rasilimali asilia zote zinazopatikana Tanzania. Rasilimali hizo huweza kuwa Misitu, mimea, gesi, milima, Wanyama, ardhi na nyinginezo. Tazama Twiga kama maliasili hapo chini Kwa maendeleo endedelevu, ni muhimu sana kuweka juhudi kwenye kuzijua, kuzitunza na kuziboresha maliasili zetu. Mfano kutunza vyanzo vya maji ni muhimu sana kwa sababu maji yanachochea maendeleo katika sekta karibia zote, hivyo maji yakitunzwa tutapata maendeleo kizazi chetu na kizazi kijacho. Aidha utunzaji wa Wanyama wetu asilia ni muhimu kwa maendeleo yetu k

Misitu yetu

Misitu ni mjumuisho wa uoto asilia wenye miti mingi ya aina mbalimbali. Misitu pia hujumuisha mime ana nyasi zinazoweza kuwa ndefu au fupi. Aina ya misitu Misitu asilia Hii ni aina ya misitu inayoota yenyewe bila kupandwa na mwanadamu. Mfano Mininga, miombo na mikoko ni aina ya misitu inayoweza kuota yenyewe bila kupandwa. Misitu ni mjumuisho wa uoto asilia wenye miti mingi ya aina mbalimbali. Misitu pia hujumuisha mime ana nyasi zinazoweza kuwa ndefu au fupi.   Misitu ya kupandwa. Hii ni misitu inayoota baada ya kupandwa na mwanadamu na kwa kiasi Fulani ukuaji wa misitu hii hutegemea juhudi zitazowekwa. Mfano wa misitu hii ni milingoti, mipaina na mikaratusi Tanzania tumejaaliwa kwa kiasi kikubwa kuwa na misitu ya aina zote (Asilia nay a kupanda). Misitu yetu imekuwa na tija kubwa sana kuhakikisha mifumo ya kimazingira inakaa saw ana pia watu huajiriwa au kujiajiri kupitia misitu yetu. Aidha Wanyama na binadamu tunategemea uoto uliopo ili kuendesha Maisha ya kila siku. M

Zao la mwani

Mwani ni zao linalolimwa kwenye maji chumvi (baharini) na kwa kiasi kidogo kwenye makutano ya maji baridi na maji chumvi (brackish water). Kuna familia na jamii mbalimbali za mwani ikiwemo spirulina, Dunaliela na Carteria. Zanzibar  husema, mwani ni zawadi ya bahari. Hii inatokana na uwepo wa mwani kiasili kwenye bahari. Nchini Tanzania Kilimo cha mwani kinazidi kuwa muhimu kwa uchumi na mapato mbadala, hasa kwa wanawake katika vijiji vingi vya pwani  IUCN Hivyo kwa watu wanaopatikana katika ukanda wa pwani kama vile Tanga, Zanzibar, pwani, Dar es salaam, Lindi au Mtwara wanayofursa kubwa ya kuwekeza katika kilimo hiki cha mwani na kukusa uchumi na mapato kiujumla.

Wajue sangala

Sangara ni Samaki kutoka kwenye familia ya latidae n ani Samaki wa maji baridi. Asili ya Samaki jamii ya sangara ni mto naili na baadhi ya mito kadhaa. Pia Samaki hawa wanapatikana kwa kiasi kidogo katika maji baridi yaliyo changamana na maji chumvi (Brackish water). Katika nchi za afrika mashariki, sangala amekuwa miongoni mwa Samaki muhimu sana kiuchumi na chakula. Sangara kama Samaki wengine ina kiasi kikubwa sana cha protini na hivyo nilshe muhimu sana. Sangara ni Samaki anaekula nyama (carnivore) na hvyo anaweza kula Samaki wenzake na kupelekea kupungua kwa hifadhi ya Samaki wengine. Sangara anao uwezo wa kukua na kufikia urefu wa mita mbili na kuwa na uzito wa kilo 200. Hivyo ni Samaki anaeweza kukua sana  Academic Nchini Tanzania Sangara wanapatikana kwa wingi ziwa viktoria. Katika ziwa viktoria wapo baadhi ya wakulima wanaofuga sangara kwa kutumia vizimba (Pens and Cages). Hivyo unayo fursa ya kuwekeza katika ufugaji wa sangara katika ziwa viktoria na kukuza uchumi. S