Skip to main content

Posts

Showing posts with the label kilimo

Mimea yetu ya matunda

Hii ni mimea inayotupatia matunda na mazao mbalimbali. Mazao ya matunda pia huweza kuwa ya asili au ya kupandwa. Mfano wa mimea asilia ya matunda ni mifenesi inayopatikana porini. Mfano wa mimea ya matunda ni miembe, mipera, michikichi, minazi, michungwa, milimao, parachichi, ndizi, michenza, mbuni, zabibu na hiliki. Mimea ya matunda inaweza kuzalisha mazao mengine kama vile Dawa, Mafuta, Juisi au viungo vya chakula. Mazao ya matunda ni chakula pendwa kwa watu mbalimbali duniani. Ulaji wa matunda unaenda sambamba sana na uimarikaji wa afya na hupunguza matatizo mengi sana ya afya. Mazao ya matunda pia ni chanzo muhimu sana cha mapato na uchumi endapo matunda yatauzwa ndani au nje ya nchi. Tanzania imejaaliwa matunda mengi sana, hivyo ni muhimu kuwekeza katika kilimo cha matunda kwa maendeleo endelevu. Makala ijayo itaangazia Mahitaji muhimu ya kilimo cha matunda.  

Sayansi ya udongo

 Coming soon

Mazao ya nafaka

Nafaka ni mbegu za mimea jamii ya nyasi ambazo hutumika kama chakula cha binadamu. Mimea hiyo hutumiwa Zaidi kama chakula cha watu duniani Nafaka hizo ni pamoja na uwele, mtama, mchele, mahindi, ngano, shayiri, ulezi. Japokuwa mazao ya nafaka ni mengi, lakini Mahindi, mchele na ngano ndio mazao yanayolimwa na kuvunwa kwa kiasi kikubwa Zaidi duniani kote. Mazao ya nafaka yanakiasi kikubwa cha wanga (carbohydrate) n ani chanzo muhimu sana cha lishe kwa watu. Vyakula vitokanavyo na mazao ya nafaka ni kama vile ugali, uji, mandazi, chapati, mkate, tambi (spanghett). Kiujumla ni kwanza mazao ya nafaka ni mazao muhimu sana duniani kote kwa sababu ndio chanzo kikubwa cha chakula na hutumiwa na watu wengi. Katika nchi ya Tanzania mikoa ya kusini imekuwa ikifanya vizuri sana katika uzalishaji wa mazao ya nafaka (mazao ya vyakula) na kusaidia kuondoa tatizo la njaa linaloweza tokea endapo chakula hakitoshi. Mazao ya chakula yanaweza kuuzwa na kuchangia katika kuongeza uchumi na mapat...

Mazao ya biashara yanayoingiza pato kubwa Tanzania

Habari mpenzi msomaji wa Makala zetu. Leo tutaangazia mazao ya biashara yanayoingiza pato kubwa hapa nchini Tanzania. Ndugu msomaji tambua kuwa kuyajua mazao haya ya biashara yanayoingiza pato kubwa, itakusaidia kuchagua zao maalum katika uwanda wa kilimo na biashara. Kitabu cha hali ya uchumi wa taifa (2018) na ofisi ya taifa ya takwimu (NBS) inaeleza kuwa tumbaku, kahawa, chai, korosho na pamba , ni mazao ya biashara yanayoingiza pesa nyingi sana za kigeni.   Tumbaku Tumbaku ni zao la biashara linalolimwa mikoa ya Ruvuma, Tabora, Mbeya, Morogoro na Iringa . Kwa mwaka 2018, zao la tumbaku liliongoza kuingiza fedha nyingi Zaidi za kigeni. Tofauti na 2018 zao hili limekuwa likiingiza pesa nyingi kwa wakulima na kukuza pato la taifa.      2. Korosho Mikoa maarufu katika uzalishaji wa korosho ni Mtwara, Lindi, Pwani, Tanga na Ruvuma . Mara nyingi korosho imekuwa ikishika nafasi ya pili katika mazao yanayo ingiza mapato kwa watanzania na serikali kiujumla. ...