Skip to main content

Posts

Showing posts with the label Misitu&Maliasili

Maliasili zetu

Utangulizi Kwa kawaida ni muhimu kukijua kitu kabla ya kukifanya au kukitumia. Ndugu msomaji karibu upate kujifunza kuhusu maliasili. Katika hii dunia, kila nchi ina maliasili zake japo tunatofautiana kwa uwingi na aina ya maliasili hizo. Na Tanzania kama nchi, tunazo maliasili nyingi sana ambazo zinatusaidia katika Maisha yetu ya kila siku. Maliasili ni nini? Maliasili ni rasilimali asilia zinazopatikana kwenye nchi husika, kwa upande wetu, ni rasilimali asilia zote zinazopatikana Tanzania. Rasilimali hizo huweza kuwa Misitu, mimea, gesi, milima, Wanyama, ardhi na nyinginezo. Tazama Twiga kama maliasili hapo chini Kwa maendeleo endedelevu, ni muhimu sana kuweka juhudi kwenye kuzijua, kuzitunza na kuziboresha maliasili zetu. Mfano kutunza vyanzo vya maji ni muhimu sana kwa sababu maji yanachochea maendeleo katika sekta karibia zote, hivyo maji yakitunzwa tutapata maendeleo kizazi chetu na kizazi kijacho. Aidha utunzaji wa Wanyama wetu asilia ni muhimu kwa maendeleo yetu k...

Misitu yetu

Misitu ni mjumuisho wa uoto asilia wenye miti mingi ya aina mbalimbali. Misitu pia hujumuisha mime ana nyasi zinazoweza kuwa ndefu au fupi. Aina ya misitu Misitu asilia Hii ni aina ya misitu inayoota yenyewe bila kupandwa na mwanadamu. Mfano Mininga, miombo na mikoko ni aina ya misitu inayoweza kuota yenyewe bila kupandwa. Misitu ni mjumuisho wa uoto asilia wenye miti mingi ya aina mbalimbali. Misitu pia hujumuisha mime ana nyasi zinazoweza kuwa ndefu au fupi.   Misitu ya kupandwa. Hii ni misitu inayoota baada ya kupandwa na mwanadamu na kwa kiasi Fulani ukuaji wa misitu hii hutegemea juhudi zitazowekwa. Mfano wa misitu hii ni milingoti, mipaina na mikaratusi Tanzania tumejaaliwa kwa kiasi kikubwa kuwa na misitu ya aina zote (Asilia nay a kupanda). Misitu yetu imekuwa na tija kubwa sana kuhakikisha mifumo ya kimazingira inakaa saw ana pia watu huajiriwa au kujiajiri kupitia misitu yetu. Aidha Wanyama na binadamu tunategemea uoto uliopo ili kuendesha Maisha ya kila sik...