Skip to main content

Kilimo cha nyanya

 Magonjwa ya nyanya

1)Bakajani wahi ( Early blight)

Ni ugonjwa wa fangasi ni ukungu unaoshambulia mimea ya nyanya kwa kiasi kikubwa. Ugonjwa huu hushambulia zaidi katika kipindi cha mvua.

Dalili za ugonjwa huu ni kua na madoa madogo madogo yenye rangi nyeusi au rangi ya kahawia kwenye majani hasa ya chini, matunda na shina. Miche midogo kwenye kitalu inaposhambuliwa hunyauka na kufa, na Miche mikubwa hudondosha majani na matunda na kunyauka kwa shina na hatimaye kufa.




Udhibiti

Hakikisha Usafi wa shamba na ng'oa masalia ya mazao na kuchoma moto mara moja baada ya kuvuna. Pia zingatia mzunguko wa mazao na pia tumia mbegu ambazo hupinga ugonjwa huu(Resistant varieties) .

Viuatilifu ambavyo vinaweza kutumika ni kama vile EVITO T 477 SC, GLORY 750 WG (MANCOZEB), CUPROCAFFARO 50 WP (COPPER OXYCHLORIDE)

2)Bakajani chelewa (Late blight)

Ni ugonjwa  hatari sana haswa kipindi cha mvua na baridi ya wastani.

Dalili za ugonjwa huu ni kuwa na mabaka makubwa yenye majimaji kwenye matunda, Shina na hata majani.

Mabaka yenye majimaji hutokea hasa sehemu ya juu ya matunda. Mimea inaposhambuliwa na ugonjwa huu hufa katika kipindi kifupi.



Udhibiti

Zingatia kilimo cha mzunguko wa mazao, hakikisha unapalilia vizuri, tumia matandazo na ondoa masalia ya mazao shambani mara baada ya kuvuna.

Viuatilifu vinavyoweza kutumika kudhibiti ugonjwa huu ni kama vifuatavyo BANKO 500 SC, CUPROCAFFARO 50 WP, EVITO na GLORY 750 WG ( MANCOZEB)

3)Madoadoa na mnyauko bacteria ( bacterial wilt)

Ugonjwa huu husababishwa na bacteria ambao husababisha mnyauko na kufa kwa mmea ghafla.

Dalili za ugonjwa huu huonekana mara tu matunda yanapoanza, Bacteria wanaosababisha ugonjwa huu huishi ardhini katika udongo kwa mda mrefu na hushambulia mimea kupitia mizizi, Au majeraha katika mimea wakati wa kuhamisha Miche kutoka kitaluni na kupandikiza, Mazingira ambayo bacteria hawa hupendelea ni hali ya joto na unyevu katika udongo.

Vimelea hawa wakishaingia katika mishipa ya mimea huziba njia za mfumo wa mzunguko wa maji katika mimea hivyo mimea hunyauka kwa haraka Bali rangi ya kijani hubakia na bila madoa. Dalili hii husaidia kutofautiaha na mnyauko fusari( fusarium wilt). Dalili nyingine ya ugonjwa huu ni kua mimea huanza kunyauka kutokea juu 



Udhibiti

Tumia nyanya zinazo stahimili mashambulizi, tumia mzunguko wa mazao wa muda mrefu, usipande nyanya katika shamba lililopandwa migomba msimu uliopita.

Dawa yenye copper hufanya vizuri katika kupunguza tatizo hili ni kama vile CUPROCAFFARO 50 WP (copper oxychloride).

4)Mnyauko fusari ( fusarium wilt)

Ni ugonjwa hatari wa ukungu/ fangasi.

Dalili za ugonjwa huu kudumaa, kubadilika rangi na kuwa njano na kahawia na kisha kunyauka. Vimelea wa ugonjwa huu huishi ardhini na hushambulia mimea kupitia mizizi, vimelea hawa hushambulia kwa kuziba mishipa ya kupashia maji na hivyo mimea kusinyaa kwa kukosa maji na hatimaye kufa. Mashambulizi ya mnyauko fusari huenda haraka kuliko magonjwa mengine ya mnyauko. Vimelea wa ugonjwa huu huahamiri zaidi katika mazingira yenye udongo wenye majimaji.

Mmea huanza kunyauka kutokea chini kwenda juu.





Udhibiti

Hakuna kiuatilifu kinachotibu ugonjwa huu kwa asilimia mia hivyo inashauriwa baada ya ugonjwa huu kujitikeza ng'oa na choma moto mimea yote iliyoathirika kisha pulizia mimea iliyobaki dawa ya ukungu.

Pia inashauriwa kutumia mzunguko wa mazao ambayo sio jamii ya nyanya.

Pia ni muhimu kudhibiti Minyoo fundo kwani hii hudhoofisha mimea na kurahisisha kupenya kwa mnyauko fusari.

Viuatilifu vifuatavyo vinaweza kupunguza athari kwa asilimia flani ni EVITO T 477 SC na GLORY 750 WG 

5)Ugonjwa wa kata kiuno ( Damping off)

Ni ugonjwa unaosababushwa na vimelea vya fangasi. Kewepo kwa msongamano wa mimea na kukosekana kwa mtiririko bora wa maji ardhini hupelekea kuenea kwa ugonjwa huu. 

Ugonjwa huu hushambulia zaidi Miche vitaluni.

Dalili za ugonjwa huu ni kunyauka ghafla kwa Miche sentimita chache kutoka ardhini. Maji yakizid ugonjwa huu huathiri zaidi.



Udhibiti

Tumia mbegu ambazo zina chanjo ya mbegu na ni vyema kabla ya kusia kuweka dawa. Chanjo ambayo ni nzuri ni SEED PLUS 30 WS kipimo ni 10g kwenye kila kilo 4 za mbegu.

Pia mara baada ya Miche kuota tumia dawa ya ukungu kama vile IVORY M 72 WP, EVITO T 477 SC na GLORY 750 WG.

Ni muhimu kufuata maelekezo ya wataalamu juu ya utumiaji wa dawa hizo.

6)Ubwiri unga ( powdery mildew)

Huu pia ni ugonjwa wa ukungu dalili zake utaona ungaunga kwenye majani na rangi ya majivu.



Udhibiti

Tumia viuatilifu kama vile EVITO T 477 SC, 

EMINENT STAR 312.5 SE na PROCURE 480 SC.

7) Magonjwa ya virusi

Magonjwa haya huambukizwa kupitia mbegu au kusambazwa na wadudu kama inzi mweupe, wadudu mafuta, binadamu na hata vifaa vya kazi.

Mashambulizi makali huonekana wakati wa joto kali na ukame.

Dalili za magonjwa haya ni kudumaa na majani kukunjamana yakipinda kuelekea juu, kutoa matawi mengi na majani kuwa na rangi ya njano, nyeupe au zambarau.

Moja ya magonjwa ya virusi ni TOMATO MOSAIC VIRUS (TMV).




Udhibiti

Ondoa mara moja mimea iliyoahambuliwa na choma moto mbali na shmaba, zingatia Usafi wa shamba, dhibiti wadudu waenezao virus hasa inzi weupe.

MATATIZO MENGINE

MATUNDA KUPASUKA

Matunda huweza kupasuka yanapokua makubwa kukaribua na muda wa kukomaa , Ipo mipasuko ya mviringo na mingine yenye sura ya nyota.

Mipasuko hii hutokana na kutokua na mpangilio mzuri wa umwagiliaji wa maji.

Hali hii hutokea zaidi wakati wa vipindi vya jua kali na mvua vinapofuatana.


Comments

  1. Very interesting,I'm now aware of the problems related to tomato production.
    Improve by providing as much details as possible.

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

Wajue sangala

Sangara ni Samaki kutoka kwenye familia ya latidae n ani Samaki wa maji baridi. Asili ya Samaki jamii ya sangara ni mto naili na baadhi ya mito kadhaa. Pia Samaki hawa wanapatikana kwa kiasi kidogo katika maji baridi yaliyo changamana na maji chumvi (Brackish water). Katika nchi za afrika mashariki, sangala amekuwa miongoni mwa Samaki muhimu sana kiuchumi na chakula. Sangara kama Samaki wengine ina kiasi kikubwa sana cha protini na hivyo nilshe muhimu sana. Sangara ni Samaki anaekula nyama (carnivore) na hvyo anaweza kula Samaki wenzake na kupelekea kupungua kwa hifadhi ya Samaki wengine. Sangara anao uwezo wa kukua na kufikia urefu wa mita mbili na kuwa na uzito wa kilo 200. Hivyo ni Samaki anaeweza kukua sana  Academic Nchini Tanzania Sangara wanapatikana kwa wingi ziwa viktoria. Katika ziwa viktoria wapo baadhi ya wakulima wanaofuga sangara kwa kutumia vizimba (Pens and Cages). Hivyo unayo fursa ya kuwekeza katika ufugaji wa sangara katika ziwa viktoria na kukuza uchumi. S

Kambale ni nani?

Kambale ni samaki wenye umbo la mkunga na wenye sharubu (whisker) katika vichwa vyao. Kambale wanapatikana nchi za Afrika na mashariki ya kati. Kambale wanaishi kwenye maji baridi ya mito, maziwa, mikondo ya maji na mabwawa. Pia kambale huweza kuishi kwenye matope au maeneo yenye maji kidogo. Kambale walianza kufugwa miaka ya 1970 katika maeneo mbalimbali ya ulimwengu kama ilivyoainishwa na  Wikipedia .    Kwa kawaida kambale wanaweza kukua mpaka kufikia urefu wa mita 1.7 na kufikia uzito wa kilo 60 kama ilivyoelezwa na  Froose . Kambale wanakula nyama pamoja na mboji. Na kutokana na ukubwa wa mdomo wa kambale, kambale anaweza kumeza nyama kubwa kiasi. Sifa za kambale Kambale hukua haraka na huweza vyakula vya aina nyingi Kambale ni wagumu na huvumilia mazingira magumu Kambale wanaweza kufugwa wengi kwa pamoja  Kambale hawazaliani kwenye mabwawa ya kufugia bali hukua tuu Kambale huweza kukaa nje ya maji kwa muda mrefu zaidi kutokana na uwe

Wajue sato

Sato ni samaki wa mwanzo kufugwa tangu miaka 3000 iliyopitta kama inavyoelezwa huko misri. Na mpaka sasa Sato ni miongoni mwa samaki anaefugwa kwa kiasi kikubwa nchi za Africa na duniani kiujumla. Sato ni samaki wanaoweza kuishi kwenye maji baridi. Samaki hawa hupatikana kwenye mito, mikondo ya maji baridi, mabawawa au maziwa na mara chache hupatikana sehemu zenye mchanganyiko wa maji chumvi na maji baridi (Brackish water) Hivyo kutokana na mazingira ambayo sato wanaweza kuishi, unayo fursa ya kuweza kufuga sato kwenye maji baridi. Mfano, unaweza kufuga samaki hawa kwenye mito, maziwa au mabwawa ya kuchimba na ya kujenga. Sato huzaliana kwa kutaga mayai. Kwa mzunguko mmoja sato mmoja ana uwezo wa kutaga mayai kuanzia 1500-2000. Na kwa kawaida sato hutaga mayai kwa mizunguko minne mpaka nane kwa mwaka. Sato pia wana uwezo mkubwa wa kuvumilia kiasi kidogo cha hewa ya oksijeni (Oxygen). Na kwa upande wa chakula, sato wana uwezo wa kula vyakula mbalimbali (Wana uwanda mpana wa vyakula).  W