Hii ni mimea inayotupatia matunda na mazao mbalimbali. Mazao ya matunda pia huweza kuwa ya asili au ya kupandwa. Mfano wa mimea asilia ya matunda ni mifenesi inayopatikana porini.
Mfano wa mimea ya matunda ni miembe, mipera, michikichi, minazi, michungwa, milimao, parachichi, ndizi, michenza, mbuni, zabibu na hiliki.
Mimea ya
matunda inaweza kuzalisha mazao mengine kama vile Dawa, Mafuta, Juisi au viungo
vya chakula.
Mazao ya
matunda ni chakula pendwa kwa watu mbalimbali duniani. Ulaji wa matunda unaenda
sambamba sana na uimarikaji wa afya na hupunguza matatizo mengi sana ya afya.
Mazao ya
matunda pia ni chanzo muhimu sana cha mapato na uchumi endapo matunda yatauzwa
ndani au nje ya nchi.
Tanzania
imejaaliwa matunda mengi sana, hivyo ni muhimu kuwekeza katika kilimo cha matunda
kwa maendeleo endelevu.
Makala ijayo
itaangazia Mahitaji muhimu ya kilimo cha matunda.
Hlw mr. Admin hopefully kilanga yusuph, you are doing well, I will pass through your all post that i can deal with.
ReplyDelete